Monday, 21 May 2012

SUBIRI HOUSE PARTY

CHIDI BENZ
Wasanii wawili wakali kutoka Tanzania wakiongozwa na nyota wa kizazi kipya,Abdhalla Mwakwiro aka chidi na Albert Mangwea wameunganisha vichwa vyao na kuingia studio tayari kwa kollabo na tayari wameshaingiza sauti zao katika wimbo huo.
Wimbo unaojulikana ''House Paty''unatajiwa kuwa wimbo mkali tena matata kutokana na kushirikiana na wasanii hao ambao wanajulikana kwa staili zao tofuati katika mziki wa kizazi kipya.
NGWAIR
Wadadisi wanasema kwamba msanii Mangwea yupo imara tena baada ya kimya kirefu na anatarajia kufunika mistari ya wimbo huo na hana budi kurudisha hadhi yake ya zamani.
Wasanii wengine kwenye wimbo huo ni mwana dada Coreen Mwamani ‘Sindi na Godzilla.‘House Part’ unatengenezwa na mtaalamu Lamar Niekamp maarufu kama Lamar wa Lamar, ndani ya Studio yake iliyopo mtaa wa kariaoko Tanzania.
Mbali na kufanya wimbo wa pamoja kama mambo yakienda vizuri wamepanga kutengeneza albamu ya pamoja, ambayo wanaamini ikikamilika itakuwa ni moto wa kuotea mbali kutokana na vichwa hivyo kushiriki.

No comments:

Post a Comment