Monday, 30 April 2012

KIDUM KUPERFOM NA MSECHU TZ

KIDUM

Msanii Kidum kutoka nchini Burundi ambaye anafanyia kazi zake za muziki humu nchini Kenya na ambaye amefanikiwa kufanya vyema hapa Afrika Mashariki kutokana na nyimbo zake,kama vile Mapenzi,Greedy ,Abambuzi haturudi nyuma aliyomshirikisha msanii Juliana kanyamozi kutoka Uganda,anatarajiwa kugonga bonge moja la show akiwa pamoja na Peter Msechu kutoka kule Tanzania. 
Show hiyo iliyopangwa kufanyika 'Mbalamwezi Beach', inatarajia kufanyika Ijumaa ya Mei 4 mwaka huu. 
Kidumu ambaye alikuwa kioo kwa msanii Peter Msechu wakati wa shindano la Tusker Project Fame, atasindikizwa na msanii huyo katika nyimbo zake atakazoziimba usiku huo.





No comments:

Post a Comment