Kampuni ya bidhaa za Sony Barani Afrika kupitia vifaa vyake vya
muziki imemteua mwanamuziki wa nyimbo za Injili nchini Tanzania, Rose
Muhando, kuwa mmoja wa mabalozi wake.Rose Muhando amepata shavu kubwa ikiwa ni dili ya kurekodi miziki na kampuni heavyweight duniani ya muziki ya Sony. Alimshukuru Mungu kwa kumpa nafasi hiyo ya kipekee, na kuwashukuru
waliomuwezesha kimuziki miaka mingi ya yeye kuwepo kwenye industry.
Uteuzi huo umetangazwa leo (10/02/2012) na Mkurugenzi wa Mambo ya Masoko, Manusha
Sarawan, katika mkutano na wanahabari uliofanyika Hoteli ya Hyatt
Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Manusha alisema mchakato wa kumpata balozi huyo ulishirikisha wanamuziki wakongwe zaidi ya 130 barani hapa. Muhando anayejulikana kwa nyimbo zake kama Nibebe, Utamu wa Yesu zinazo tumika kama ringtones na wengi Afrika Mashariki.

No comments:
Post a Comment