Thursday, 23 February 2012

BABY MADAHA AJIUNGA NA TMK- WANAUME HALISI

Mwanadada aliyeibuka kwenye shindano la Bongo Star Search, Baby Madaha, amejiunga rasmi kwenye Kundi la TMK Wanaume Halisi Kujiunga TMK kumethibitishwa na mwanadada huyo pamoja na kiongozi Juma Kassim Ally Kiroboro  aka ‘Sir Nature’.

Mwanadada huyo ambaye atakuwa wa kike pekee kwa kundi hilo alipoulizwa alikiri kufanya kazi na TMK Wanaume Halisi na kuongeza kwamba mwaka huu ameamua kujipanga vyema zaidi.

Kwa upande wa Nature, alijibu: “Unauliza maembe kibada? Baby Madaha ndiye first lady wa Halisi. Tumemchukua kwa sababu anaweza kazi.” Baby alifanya kazi mbalimbali ndani na nje ya nchi lakini alipotoa ngoma yake inayokwenda kwa jina la Amore, ilimtambulisha vema.

No comments:

Post a Comment