Monday, 20 February 2012

AMINI WA "THT" TAABANI?

AMINI
Msanii huyu anakwenda kwa jina la Amini Mwinyimkuu ‘Amini’ aliyekuwa kwa kundi la THT. Inafaamika  kwamba msela huyu huenda akatimuliwa ndani ya kundi hilo kutokana na utovu wa nidhamu.

Akiongea Amini alisema kikubwa kinachotaka kumfukuzisha hapo ni kuchukia tabia za baadhi ya wasanii wa kundi hilo ambao wanajipendekeza kwa mabosi. Msanii huyu alisema si kweli kuwa ana nidhamu mbovu kama inavyodaiwa lakini kutokana  na hulka yake ya kupenda kusimamia ukweli kwenye kila jambo basi amekuwa akionekana mkorofi.

Mpaka anaongelea swala hili uongozi wa THT ulikuwa unataka kukaa kikao kumjadili kwamba afukuzwe au abaki.“Yani nimesikia kwamba najadiliwa na uongozi wa kundi ili niweze kufukuzwa lakini kwa upande wangu sioni kama ni tatizo kwa sababu kama kipaji ninacho hivyo nasema kama mimi ni mtovu wa ni nidhamu sawa niko tayari kuondoka,” alisema.

No comments:

Post a Comment