Friday, 10 February 2012

20% AKWEPA KUWA MGENI WA SERIKALI

20%
Msanii 20 percent awakera mashabiki wake kwakunaswa na polisi akiwa na dawa za kulevya aina ya bangi na kuhukumiwa miaka saba ama kulipa faini ya shilingi laki mbili.kwa mjibu wa reporti zinazo fikia meza yetu ya ketauexpress toka Bongo.
Hakimu wa mahakama ya wilaya Kilwa mheshimiwa Arcado Chuwa alitoa hukumu hiyo baada ya kukamilisha kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, za utetezi na mashataka.Alisema ili kuwa fundisho kwa wengine baada ya mahakama kumtia hatiani anamhukumu kifungo cha miaka saba au faini ya sh 200,000.Hata hivyo 20 percent alikwepa kifungo baada ya kulipa kiasi hicho cha fedha .

Awali mwendesha mashitaka Inspector wa jeshi la polisi, wilayani Kilwa, Thomas alisema mtuhumiwa alikutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi gramu 20 mwaka jana mwezi wa Desemba wakati akiwa safarini kwenye kijiji cha Nangurukuru katika gari lake, wilayani Kilwa.

No comments:

Post a Comment